Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Usafiri Ardhini

Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Usafiri Ardhini

Karibu

Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za Usafiri Ardhini (LATRA CCC) tunapenda kukukaribisha katika tovuti yetu hii.

Baraza lilianzishwa kwa kifungu cha 29 cha Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA) Na. 3 ya mwaka 2019 likipewa uwezo kisheria kuwa kiungo baina ya watumiaji wa huduma zinazodhibitiwa na Mamlaka ya LATRA, watoa huduma, LATRA yenyewe,serikali na watunga sera na miongozo mbalimbali ya Usafiri Ardhini nchini.

Tukiwa na miongozo inayohakikisha Uadilifu, Uwazi, Uwajibikaji, Ubunifu, Kuzingatia matokeo,  Uitikio wa haraka; tunajipambanua kuihusisha jamii katika kupata mrejesho na maoni ili kufikia kuwa na usafiri wa ardhini ambao ni wa kufaa kutegemewa, salama, kwa wakati, bei nafuu na rafiki kwa mazingira.

Tunajitahidi kufikia kuwa na usafiri wenye viwango vya juu kwa mabasi ya mijini (daladala), mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi, taxi, pikipiki za magurudumu mawili na matatu pamoja na usafiri kwa njia ya reli bila kusahau usafiri kwa njia ya kamba.

Karibu sana kwa mawasiliano shirikishi na Baraza kupitia:

Baruapepe: barua@latraccc.go.tz

Akaunti za Mitandao ya Kijamii: Intagram, Facebook, Youtube, Twitter:  @latraccctz

Simu Na :  0736 11 00 20

                    0800 11 10 80 [Piga Bure]

 

                     KAULI MBIU:

“LATRA CCC, SAUTI YA JAMII, USAFIRI BORA ARDHINI

ASANTE KWA KUTEMBELEA TOVUTI YETU!